Vita ya wababe wawili EPL kwa koulibaly
NAPLES ITALIA. VITA ya kunasa huduma ya beki wa kati wa Napoli, Kalidou Koulibaly imeripotiwa kubaki kwa timu mbili pekee kwa sasa, miamba ya Ligi Kuu England, Manchester United na Liverpool.
Jambo hilo limekuja baada ya mabingwa wa soka wa Ufaransa, matajiri Paris Saint-Germain kuripotiwa kujitoa kwenye mbio za kumnasa Msenegali huyo.
Awali, PSG walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kunasa saini ya Koulibaly, lakini kujitoa kwao kunafanya Liverpool na Man United kubaki wenyewe wenye nguvu kubwa ya kumshawishi beki huyo akaenda kujiunga na timu zao.
No comments