Uingereza yapitisha sheria ngumu
London,Uingereza. Ushiriki wa timu za Manchester City, Chelsea na Manchester United katika mashindano ya Ulaya msimu huu umewekwa kwenye mabano baada ya serikali ya Uingereza kupitisha sheria ngumu inayoweza kuziathiri.
Sheria hiyo ni ya wasafiri wote wanaoingia nchini humo kuwekwa karantini kwa siku 14 (wiki mbili) na baada ya hapo ndipo waendelee na shughuli nyingine zilizowapeleka nchini humo.
Uamuzi huo umeonekana utaziletea shida Manchester City na Chelsea zinazoshiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya na Manchester United iliyopo katika Kombe la Europa kwani utavuruga ratiba zao au za wapinzani wao katika mashindano hayo.
No comments