Breaking News

Kisa yanga, Nchimbi aongezwa Taifa stars

BAADA ya kuifunga Yanga mabao matatu 'hat-trick' mshambuliaji wa Polisi Tanzania, Ditram Nchimbi ameongezwa kwenye kikosi cha timu ya taifa 'Taifa Stars' kinachotarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Rwanda.
Nchimbi ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuitwa Stars ameungana na nyota wengine 28 waliotajwa jana Alhamis na kaimu kocha mkuu wa Stars, Etienne Ndayiragije kujiandaa na mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa Oktoba 14 mwaka huu mjini Kigali.

No comments