Uwanjani maumivu lakini mapato yaongezeka

Mapato ya Manchester United yameongezeka kwa rekodi mpya ya kiwango cha £627m kwa mwaka kufikia Julai.
Hii ni licha ya klabu hiyo kukabiliwa na msimu mgumu wa 2018-19 liochangia kuondoka kwa meneja Jose Mourinho na timu hiyo kumaliza msimu ikiw akatika nafasi ya sita.
Mapato yanayotokana na matangazo ya biashara yaliimarika kwa 18%, kutokana na mkataba mpya wa Uefa ya ligi ya mabingwa, huku mauzo ya kibiashara yakisalia kama yalivyokuwa.
Lakini timu hiyo inatarajia mapato na faida kushuka katika msimu wa 2019-20 baada ya kushindwa kufuzu katika ligi ya mabingwa msimu huu.

No comments